Friday, August 7, 2009

Label ya kutoka Tanzania

Juzi nilipitia kwenye duka la Lidl kutafuta bidhaa mbalimbali, zikiwemo na chakula. Katika kupitia mashelf mbalimbali nikaona hii T shirt yenye label ya Serengeti. Nikafurahi kuona jina la nyumbani, na nikahisi labda imetoka kwetu nyumbani . Kuichunguza kwa karibu nikaona kuwa imetengenezwa Ujerumani. Sijui sana mambo ya kisheria, hivyo nikabaki nimeduwaa, je ni vipi hawa jamaa kutumia majina yetu, ni sawa?

No comments: