Monday, February 11, 2008

FEST AFRICA 2008

FEST AFRICA 2008


DEAR FRIENDS
FEST AFRIKA PRESENTS AN AFRICAN WINTER JAM FESTIVAL. SPICED WITH LOTS OF HAPPENINGS AND GREAT LIVE EVENTS. ATTACHED BELOW IS THE PROGRAMME, PLEASE GO THROUGH IT. COME ONE COME ALL. TICKETS ON SALE IN ADVANCE (check below), PLEASE HURRY AND DON'T MISS A CHANCE TO PARTICIPATE IN THE BEST AFRICAN EVENT OF THE YEAR. PLEASE FORWARD TO FRIENDS.


DATE : SATURDAY 23.02.2008
TIME : 20-04:00
PLACE: KLUBI-TAMPERE-FINLAND


SUPPORTING ARTISTS :-

.PAPA ZAI-FROM ZAMBIA - ROOTS REGGAE SOUND SYSTEAM.
.CHEZA NGOMA - Fin -Tanzania-Afro dance.
.SAMBA GIRLS -Fin-
Oba oba.
.
OCG-Tanzania
RnB and HipHop.
.MPONDA´S-
Singing, drumming and body movements.

MAIN BAND


.PABLOMACHINE and THE TANGANYIKA SOUND- From Tanzania & Burundi (based in Sweden)

Plays Ndombolo, Afro-Rumba, Soukous, Afro-Beats & much more


DJs CLIFF (dj hakuna matata)
Fidelis- Sweden
Mambo Team


TICKETS 10€ Advance at Klubi, Epe´s and Swamp Music;
15€ at the door


Links:

www.festafrika.net
www.pablomachine.podomatic.com
www.bredband.net
www.chezangoma.net

Friday, January 18, 2008

JETFIGHTER


Unaweza kujifunza kuwa fundi wa jetfighter!

Friday, January 11, 2008

CATHEDRAL LA TAMPERE

FILOSOFIA

Nimeshasoma maneno mengi yaliyojaa filosofia nzuri, na natumaini wengi wenu mmeshayasoma pia. Kuna nmaneno fulani niliyaona yamebandikwa kwenye ukuta wa sebule wa nyumba moja hapa Tampere, ambayo yalinifanya nitafakari sana. Labda na wewe yatakufanya utafakari. Maneno yenyewe yalikuwa katika lugha ya kiingereza, na yalikuwa kama yafuatavyo:

"ALL VISITORS WHO COME TO THIS HOUSE MAKE US VERY HAPPY, SOME WHEN THEY ARRIVE AND SOME WHEN THEY LEAVE"

Upo hapo?

Na katika pitapita zangu leo katika mitaa ya Tampere niliona jamaa kaandika haya maandishi katika mojawapo ya mabin ya mjini. Nikafikiria ni kitu gani kilichomfanya jamaa huyu kuandika haya maneno, tena kwa ufanisi mzuri. Nikatafakari, nikasema; "Mmhhh". Wewe je?




Monday, December 31, 2007

HERI ZA MWAKA MPYA 2008

KWA NIABA YA WATANZANIA WAISHIO TAMPERE, NAPENDA KUWATAKIA WADAU WOTE WA BLOG HII HERI NA FANAKA ZA MWAKA MPYA 2008!

Wednesday, December 26, 2007

KRISMASI YA 2007

Mwaka huu sikukuu ya Krismasi ilisherehekewa kwa ujumla nyumbani kwa Dr. Augustino Binamu ambapo wadau wengi walihudhuria. Picha zitajieleza zenyewe!


Dr. Augustino Binamu (kulia)

Monday, December 10, 2007

SHULE ZA TAMPERE

Hapa Tampere kuna shule nyingi ambazo zinatoa mafunzo mbalimbali. Hapa ni kwenye shule ambayo inafundisha vijana waliohitimu mafunzo ya sekondari kujofunza umekanika wa ndege. Finland kuna nafasi nyingi sana za masomo, na hivi karibuni vijana wengi wa ki Tanzania wamekuwa wakichangamkia nafasi hizo. Kitu kizuri zaidi ni kuwa hakuna gharama zozote za ada!

Tuesday, December 4, 2007

MGENI KUTOKA MWANZA

Pichani ni Mwalimu WINFRIDA MASANJA kutoka shule ya Igoma, Mwanza, ambaye kwa sasa yupo Tampere kutembelea shule za hapa mjini katika mpango maalum wa urafiki kati ya mji wa Mwanza na Tampere.

Wednesday, November 28, 2007

MENARD MPONDA, U WAPI?

Naitwa Alex Rwambali nipo GERMANY; tafadhali naomba contact za MEDAD MPONDA huyo jamaa tulikuwa nae pale Bagamoyo miaka ya 1993-1995 alinitangulia mwaka mmoja. Email yangu hiyo hapo.Nashukuru in advance
amagere@hotmail.com

November 27, 2007 5:30 PM

USIKU WA MWAFRIKA, JOENSUU

Naitwa Sunday Ngakama toka Mwanza, ninapenda kuwajulisha Watanzania wote waishio Finland kwamba kutakuwa na usiku wa Mwafrika tarehe 28 Novemba, katika ukumbi wa jiji la Joensuu, Teatteri Klubi.

Kwa maelezo zaidi, mawasiliano kwa: sundayngakama@yahoo.co.uk, au 0505373949. Asanteni!

Sunday, November 18, 2007

MWANZA NITE

Hapo jana, tarehe 17 Novemba 2007 katika ukumbi wa KLUBI kulikuwa na sherehe za kuadhimisha Mwanza Day. Sherehe hizo zilifanikishwa na muziki wa disko (ngwasuma, bongo flava n.k.) uliopigwa na DJ George Matovu, nyimbo na ngoma za vijana wa Mponda (hatuondoki mpaka pombe iishe) , ngoma na muziki wa kantele ulipigwa pia na kikundi cha Bandu Bandu kikiongozwa na Arnold Chiwalala. Vijana wa Cheza ngoma walifurahisha watazamaji kwa ngoma zao mbalimbali, hasa ile ya gobogobo. Bendi ya Galaxy (wanamuziki wa Senegali) kutoka Helsinki walifurahisha pia watazamaji kwa muziki wao wa Senegal hasa kutokana na ile ngoma yao inayoteta.

George Matovu


Mpondas


Bandu Bandu


Galaxy on stage



Klubi

Wageni kutoka Mwanza






Sunday, November 11, 2007

GRADUATION PARTY YA ROBERT MHEKWA

Tarehe 10 Novemba 2007, siku ya Jumamosi tulijumuika pamoja kusherehekea graduation ya ndugu yetu Robert Mhekwa pale alipochukua nondoz zake. Picha zenyewe zinajieleza.


Robert Mhekwa (kushoto)



Tuesday, October 16, 2007

AUTUMN IMEWADIA

Kipindi cha autumn kimewadia kwetu. Katika kipindi hiki, baridi huanza kuwa kali, majani hupukutika kutoka mitini na jua linachelewa kuchomoza asubuhi, na kuzama wakati wa adhuhuri. Matokeo yake ni kuwa katika giza kwa muda mrefu zaidi. Ili kuchangamsha nafsi za watu, kunakuwa na mapambo ya taa katika barabara kubwa ya Tampere, Hameenkatu.

Hameenkatu leo saa 5 asubuhi (16/10/2007)

Saturday, September 29, 2007

MNADA WA POLISI

Leo kuanzia saa sita mchana palikuwepo na mnada wa Polisi ambapo vitu vingi vilinadiwa. Vitu hivyo vilikuwa baiskeli, navigators, playstation, simu na kadhalika. Mnada kama huu hufanyika kila mwaka wakati kama huu na unaweza kujipatia kifaa kizuri kwa bei ya mnadani. Niliona wanafunzi Wachina na Wahindi ambao walinunua baiskeli.

Thursday, September 27, 2007

Monday, September 24, 2007

KARIBUNI

Karibuni katika blog hii kutoa maoni, matangazo kuweka picha na kadhalika.